Ushindi Wa Taabu wa Mancheser United na Msimamo Wa Ligi Kuu England.

Klabu ya Manchester United imepata ushindi wa goli 3-2 na kukwea hadi katika nafasi ya pili ya msimamo wa ligi baada ya kuwanyuka kwa mbinde Tai wa Uingereza (Crystal Palace).

Walikuwa ni Crystal Palace waliotangulia kuliona lango la Manchester United mnamo dakika ya 11' kupitia kwa Townsend na kuongeza bao la pili mnamo dakika ya 48' kupitia kwa Van Aanholt.

-Manchester wanazinduka kutoka katika dimbei zito la usngiza mbamo dakika ya 55 na kupata bao la kwanza kupitia kwa Chris Smalling na Lukaku kufunga bao la kusawazisha mnamo dakika ya  76 kabla ya Matic kupigilia msumali wa mwisho kwenye jeneza la Crystal Palace mnamo dakika za jioni kabisa 90+1'.

Ka goli alilofunga Lukaku limemfanya afikishe magoli 14 akishika nafasi ya tano katika orodha ya wake wenye magoli mengi England.

No comments:

Note: only a member of this blog may post a comment.