Ratiba Ya Mechi Ya Simba Na Al Masry Yapanguliwa.

Shirikisho la mpira wa miguu Barani Afrika (CAF), limefanya mabadiliko ya ratiba katika baadhi ya michezo ikiwemo wa Simba dhidi ya Al Masry SC katika Kombe la Shirikisho.

Awali mechi hiyo ilipangwa kupigwa Match 6 mwaka huu na Simba wakianzia nyumbani, baada ya mabadiliko mchezo huo utafanyika March 9-2018 baada ya tarehe ya mwanzo kufanana na mechi ya Yanga.

Baada ya mabadiliko hayo, sasa Simba wataanzia nyumbani kama ilivyokuwa mwanzo na mchezo wa marudiano ratiba inaonesha mchezo utapigwa March 16 2018, huko Misry

No comments:

Note: only a member of this blog may post a comment.