Azam Warejea Mazoezini Kuwawinda Mwadui FC.

Baada ya mapumziko ya siku moja, kikosi cha Azam FC, kimerejea mazoezini tayari kujiandaa na mchezo ujao wa ligi dhidi ya Mwadui fc.

Azam wanatarajiwa kuteremka dimband kumenyana na Mwadui katika mchezo utakaofanyika Uwanja wa Azam Complex Alhamisi hii saa 1.00 usiku.

Mchezo huu unatarajiwa kuwa wa aina yake kwani timu zote mbili zinahitaji ushindi ili kujiweka katika nafasi nzuri katika msimamo wa ligi ambapo Azam watakuwa wanawanyatia Yanga ambao wapo katika nafasi ya pili na hata kuwanyatia vinara wa ligi hiyo Simba ili kutwaa ubingwa.

No comments:

Note: only a member of this blog may post a comment.