Mbeya City Na Mwadui Hakuna Mbabe..


Mchezo uliowakutanisha wanakomakumwanya Mbeya City na wachimba almasi Mwadui FC umemalizika kwa suluhu ya 0-0, mchezo ukifanyika katika uwanja wa Sokoine jijini Mbeya.

Mchezo huo ulianza mapema kabisa mishale ya saa nane mchana ili kupisha mchezo wa kiporo kati ya Tanzania Prisons na Mbao ambao wenyewe ilibidi kuanza saa kumi baada kushindwa kufanyika saa nne asubuhi.

Matokeo hayo yanawafanya Mbeya City kufikisha alama 21 na kuendelea kuwa katika 10 wakati Mwadui wanafikisha alama 20 katika nafasi ya 9 ya msimamo wa ligi kuu soka Tanzania Bara.

No comments:

Note: only a member of this blog may post a comment.