Simba, Mo wamalizana kibingwa


Leo Jumapili Mei 20, 2018 klabu ya Simba imefanya mkutano mkuu wa dharura kwa ajili ya mabailiko ya katiba yao ili kuendana na mfumo mpya wa uendeshaji wa klabu hiyo.
Wanachama wa Simba kwa pamoja wamepiga kura ya ndio kupitisha mabadiliko ya katiba yao ili kubadilisha mfumo wa uendeshaji wa klabu ambapo kuanzia sasa klabu hiyo itaendeshwa kwa mfumo wa hisa.
Mwekezaji Mohamed Dewji amechukua hisa asilimia 49 na wanachama wengine wamebaki na hisa 51%.

No comments:

Note: only a member of this blog may post a comment.