+ PICHA: Wababe Wa Yanga Watua Salama Gaborone Botswana...


Maea baada ya kuinyuka klabu ya Yanga wachezaji na uongozi wa klabu ya Township Rollers hatimaye wamesawasili mjini Gaborone nchini Botswana usiku huu.

Township Rollers waliondoka Tanzania kwa ndege na kupitia Afrika Kusini ambapo waliondoka nchini majira ya saa tisa alasiri  15:00 ambao ni sawa na saa 14:00 kwa majira ya GabGrone na kuwasili Johannesburg majira ya saa kumi na mbili jioni 18:00.


Klabu hiyo ilianza safari ya kutoka Johannesburg majira ya saa mbili usiku 20:00 na kutua Gaborone nchini Botswana majira ya tatu 21:00 usiku.

Shamrashamra za mashabiki waliojitikeza kuipokea klabu hiyo na ushindi zilitapakaa katika viunga vya mjibwa Gaborone hasa maeneo ya uwanja wa ndege walipofikia vijana hao.

Picha: Hivi ndivyo walivyowasili nyumbani kwao Gaborone nchini Botswana.












Ikumbukwe kuwa klbu hiyo baada ya mchezo dhidi ya Yanga inatarajiwa kushuka dimbani tena kuwa kabili BlackFores FC.

No comments:

Note: only a member of this blog may post a comment.