Niyonzima Arejea Tanzania Bila Kufanyiwa Upasuaji.


Kiungo wa klabu ya Simba SC, Haruna Niyonzima amewasili ncgini akitokea India likokwenda kutibiwa, kwa mujibu wa taarifa rasmi kutoka kwa mkuu wa idara ya habari na mawasiliano wa Simba SC Haji Manara amethibitisha kuwa Nyonzima amerudi nchini.


Haruna Niyonzima anarejea Tanzania ikiwa ni wiki kadhaa zimepita toka akosekane uwanjani, kwa kile kilichodaiwa kuwa ni kuhitaji kufanyiwa upasuaji baada ya mfupa wa mguu wake kugundulika kuwa ulikuwa na ufa wa muda mrefu.


Niyonzima amerudi Tanzania akitokea India bila kufanyiwa upasuaji mdogo kama ilivyokuwa imeripotiwa awali, baada ya madaktari India kumpatia tiba mbadala iliyotatua tatizo lake na kumfanya arudi katika hali yake ya kawaida pasipo kuhitaji kufanyiwa upasuaji.

No comments:

Note: only a member of this blog may post a comment.