Manara Akanusha Aveva Kulazwa ICU..

Afisa habari wa klabu ya Simba sc, Haji Manara amekanusha taarifa zinazoeleza  kuwa aliekuwa raisi wa klabu hiyo Evans Aveva kalazwa katika kitengo cha wagonjwa mahututi kunko Hospitali ya taifa ya Muhimbili.

Kwa mujibu wa taarifa iliyoenezwa kwenye mitandao ya kijamii leo ni kuwa raisi huyo amelazwa kutokana na hali yake kutokuwa nzuri.

Hayo yameelezwa leo Machi 8 mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Wilbard Mashauri na wakili anayewatetea, Evodius Mtawala wakati kesi hiyo ilipotajwa mahakamani hapo.

“Mshtakiwa wa kwanza Aveva, tangu jana amelazwa katika kitengo cha wagonjwa mahututi hali yake siyo nzuri," ameeleza wakili Mtawala.

Sasa kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa Manara akizungumza na East Afrika Radio amesema Aveva Hayuko kwenye chumba cha wagonjwa mahututi "ICU"..

No comments:

Note: only a member of this blog may post a comment.