Kocha Township Rollers"Nalijua Soka La Afrika"

Kocha wa klabu ya Township Rollers ya Botswana, Nikola Kavazovic amesema analijua soka la Afrika. Kavazovic amesema amekuwa akilifuatilia vizuri soka la Afrika, na timu yake ipo tayari kupambana na wapinzani katika mchezo wa kesho.


Licha ya kulijua soka la Afrika, Kavazovic, amesema amekuwa akiifuatilia pia Yanga katika michezo mbalimbali ya kimataifa iliyocheza, huku akieleza ameshaitazama ikicheza miwili ya nyumbani na miwili ya ugenini.

"Nalijua vizuri soka la Afrika, nimekuwa nikilifuatilia. Tupo tayari kwa mchezo wa kesho maana nimeifuatilia pia Yanga mechi kadhaa ilizocheza ugenini na hapa nyumbani" - Nikola Kavazovic (Kocha wa Township Rollers FC).

Licha ya kuifuatilia Yanga, Kavazovic
Township Rollers itacheza mchezo wa kesho baada ya kuwaondoa Al Merrikh katika mchezo uliopita.05Mar2018



No comments:

Note: only a member of this blog may post a comment.