YANGA TUMIENI MUDA HUU KUBADILI UPEPO



INAFAHAMIKA wazi kwamba hivi sasa Yanga imekuwa haina ma­tokeo mazuri kwenye michuano inayoshiriki tangu kuondoka kwa aliyekuwa kocha wao mkuu, George Lwandamina raia wa Zam­bia.



Tangu kuondoka kwa Lwandami­na katikati ya mwezi uliopita, Yan­ga imeshindwa kupata matokeo mazuri katika mechi zake nane za kimashindano ilizocheza mpaka sasa, Ligi Kuu Bara na Kombe la Shirikisho Afrika.



Kabla ya hapo, matokeo ya Yan­ga kwenye mechi zake yalikuwa hivi; Yanga 1-1 Singida, Wolaita Dicha 1-0 Yanga, Simba 1-0 Yanga, Mbeya City 1-1 Yanga, USM Alger 4-0 Yanga, Prisons 2-0 Yanga, Mti­bwa 1-0 Yanga na Yanga 0-0 Rayon Sports.



Matokeo hayo si mazuri ikizingati­wa kwamba Yanga ndiyo mwakili­shi pekee kimataifa hadi sasa ngazi ya klabu.

Tunafahamu kwamba tangu kuon­doka kwa Lwandamina kumeibu­ka mambo mengi ikiwemo migo­mo kwa wachezaji wakishinikiza kulipwa maslahi yao jambo am­balo kwa kiasi fulani limechangia matokeo mabaya kwa timu hiyo.



Baada ya mchezo wa juzi wa Kombe la Shirikisho Afrika, Yan­ga haitacheza tena mpaka Julai 17, mwaka huu itakapocheza dhidi ya Gor Mahia ya Kenya, hivyo kipindi hiki cha mwezi mmoja kilichopo hapa kati, lazima kifanyike kitu cha kipe­kee ili kubadilisha mwelekeo wenu.



Yafanyike maandalizi ya maa­na, pia kuondoa zile tofauti zenu zilizopo ndani ya klabu ili timu iweze kufanya vizuri. Nadhani muda huu uliopo unatosha kabisa kufanya ma­badiliko hayo

No comments:

Note: only a member of this blog may post a comment.