Kagera Sugar Wavunja Rekodi Ya Simba VPL 2017/2018


Baada ya michezo 28 bila kupoteza hatimaye Simba yakubali kichapo cha goli 1-0 kutoka kwa Kagera Sugar katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Mchezo huo haukuwa rahisi mbele ya Rais John Pombe Magufuli na kuifanya Simba ipoteze kwa mara ya kwanza katika uwanja wa Taifa Dar es Salaam.

Hata hivyo Simba ilifanikiwa kupata penati katika dakika za majeruhi, lakini penati hiyo ilipanguliwa na aliyekuwa kipa wa Simba Juma Kaseja.

Juma Kaseja imeonekana kama aipotezea Simba baada ya kupangua penati ya Emanuel Okwi na kuweka historia nzuri ya kuifunga Simba timu yake ya Kagera.

Hii imetokea kama ilivyokuwa Barcelona baada ya kukubali kichapo cha magoli 5-4 dhidi ya Levante.

No comments:

Note: only a member of this blog may post a comment.