TETESI: Simba Yawanyatia Kwa Karibu Nyota Hawa Ligi Kuu Tanzania Bara.

Wakati dirisha la usajili wa wachezaji kwa msimu wa mwaka 2018/2019 likikaribia kufunguliwa tayari tetesi za baadhi ya wachezaji kuhama zimeanza kuanikwa wazi.

Wachezaji ambao tayari wameanza kuzungumzwa ni pamoja na Obrey Chirwa wa Yanga na Adam Salamba wa Lipuli.

Pamoja na hao pia kiungo machachali wa klabu ya Singida United amekuwa miongoni mwa wachezaji ambao wamekuwa wakihusishwa kujiunga na wekundu hao wa msimbazi.

Klabu hiyo imeeleza kuwa nia ya kuwasajili nyota hao ni kuweka imara kikosi chao ili kuhakikisha wanapambana vyema katika mashindano ya kimataifa hususani klabu bingwa Afrika kwani wanaamini kuwa wao ndio mabingwa msimu huu.

No comments:

Note: only a member of this blog may post a comment.