Saleh: Tshishimbi Kurejea Dimbani Hivi Karibuni

Meneja wa Yanga Hafidh Saleh amesema kiungo Papi Tshishimbi alipata maumivu katika mguu wake yaliyomfanya ashindwe kumaliza mchezo dhidi ya Wolaitta Dicha.

Kwenye mchezo huo ambao Yanga ilichapwa bao 1-0 lakini ikafuzu hatua ya makundi kwa ushindi wa jumla wa mabao 2-1, Tshishimbi alitolewa kwenye dakika ya 67 na nafasi yake kuchukuliwa na Emanuel Martin.

Saleh amesema wanatarajia kiungo huyo ataweza kurejea dimbani kuzikabili Mbeya City na Simba kwenye michezo inayofuata.

No comments:

Note: only a member of this blog may post a comment.