HASPOPPPE AUNGANISHWA NA AVEVA,KABURU KESI YA UTAKATISHAJI
Hakimu mkuu wa mahakama hiyo, Thomas Simba amelitaka jeshi la polisi kumkamata mara moja Hanspoppe kwani ameonekana kuhusika moja kwa moja kwenye kesi hiyo inayowakabili Rais wa klabu ya Simba, Evans Aveva na makamu wake Geofrey Nyange "Kaburu" ambao wanasota mahabusu hadi sasa.
Hanspoppe naye amehusishwa kwenye kesi hiyo ya utakatishaji fedha za klabu ya Simba zinazokadiliwa kufikia dola 300,000 za Kimarekani, kwa mujibu wa wakili wa Taasisi ya kupambana na rushwa nchini, (TAKUKURU) Leonard Swai amebadilisha hati ya mashitaka na kuliingiza jina la Hanspoppe pamoja na Franklin Lauwo ambapo wote hao watapelekwa na polisi na sasa wametakiwa kukamatwa
Amri hiyo imetolewa na Hakimu Mkazi Mkuu Thomas Simba baada ya Wakili wa TAKUKURU, Leonard Swai kubadilisha hati ya mashtaka na kuwaongeza watuhumiwa hao.
Swai amedai amewatafuta washtakiwa hao toka mwezi wa tatu bila mafanikio na kuomba hati ya kuwakamata washtakiwa hao ambao hawakuepo mahakamani.
Washtakiwa hao wameongezwa katika kesi ya utakatishaji fedha na kugushi inayomkabili Rais wa Simba, Evans Aveva na makamu wake, Geofrey Nyange ‘Kaburu’ .
No comments:
Note: only a member of this blog may post a comment.