Hii Hapa Zawadi Aliyopewa Mh. Rais Magufuli Na Klabu Ya Simba.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk.John Magufuli amepewa zawadi ya jezi na klabu ya Simba katika mkutano mkuu wa dharura unaoendelea katika ukumbi wa Mwalimu Nyerere.

Zawadi hiyo imepokelewa na Waziri Habari Sanaa Utamaduni na Michezo Dk. Harrison Mwakyembe ambaye amehudhuria mkutano huo.

Rais wa Magufuli aliwakabidhi Simba kombe la ubingwa jana katika uwanja wa Taifa baada ya kumalizika kwa mechi ya ligi kati yao na Kagera Sugar.

Mkutano huo wanajadili mabadiliko ya katiba ili kubadili mfumo wa uendeshaji kutoka umiliki wa wanachama kwenda kwenye hisa.

Bilionea Mohammed Dewji ameshinda zabuni hiyo na anategemewa kuweka hisa asilimia 49 zenye thamani ya sh billioni 20 kama utaratibu ukikamilika.

No comments:

Note: only a member of this blog may post a comment.