WATUKUTU WA 2016/2017 WALIVYOTOBOA


Ligi kuu Tanzania bara msimu wa 2017/2018 inaelekea ukingoni huku wachezaji kadhaa wakiwa wameonyesha viwango vyao na wanaimani ya kucheza soka la kulipwa nje ya nchi.

Mwaka jana wakati msimu wa 2016/2017 unaelekea tamati kuna wachezaji kadhaa walionyesha vitendo vya utovu wa nidhamu.

Baadhi ya wachezaji hao ni pamoja na Abdi banda aliyekuwa akichezea Simba, Simon Msuva na Deogratius Munishi "DIDA" wote walikuwa wanaichezea klabu ya Yanga.

Abdi Banda alimpiga beki wa kagera sugar George Kavila kwenye mchezo ambao Simba ilifungwa mabao 2-1, tukio hilo lilipelekea kufungiwa michezo mitatu na kamati ya nidhamu ya TFF.

Simon Msuva na Deogratius Munishi "DIDA" walionywa na kamati ya nidhamu baada ya kufanya kosa la kumzonga na kumtolea muamuzi maneno machafu kwenye mchezo wao wa mwisho wa ligi kuu dhidi ya Mbao Fc mchezo ambao Yanga ilifungwa bao 1-0.

Baada ya ligi kuu kumalizika zikaanza tetesi za wachezaji hao kutakiwa na timu za nje ya nchi, na baada ya tetesi za muda mrefu hatimaye wachezaji hayo wakaiaga ligi kuu Tanzania bara kwa muda.

Banda akasajiliwa na Baroka Fc ya Afrika kusini, Msuva akasajiliwa na Difaa Al Jadida ya Morocco na Dida akasajiliwa na University of Pritoria ya Afrika kusini

Join us on WHATSAPP Usipitwe Na Breaking News Za Soka: Jiunge nasi kupitia Facebook, Bofya LIKE Button...

No comments:

Note: only a member of this blog may post a comment.