Masau Bwire: Tutaendelea Kutumia Mfumo wetu wa kupapasa


Wakati ikingojewa ligi kuu Tanzania irejee baada ya kusimama kwa muda kupisha kalenda ya FIFA, Mwandishi wetu, Alexander Victor leo amefanikiwa kuzungumza na Afisa habari wa klabu ya Ruvu Shooting, Masau Bwire naye kuelezea maandalizi ya klabu yake kuelekea mchezo dhidi ya Tanzania Prisons.

Masau akizungumza na mwandishi wetu amemueleza kuwa timu yake inaendelea vyema na maandalizi ya michezo ijayo ya ligi kuu zaidi zaidi akiuzungumzia mchezo dhidi ya Tanzania Prisons ambao utapigwa kunako uwanja wa Mabatini mnamo aApril 8.

"Tutakuwa na mchezo tarehe 08.04.2018 mchezo ambao tutachezea nyumbabi kwetu na tunakwenda kucheza na timu kubwa ambayo kwa siku za hivi karibuni imekuwa ikifanya vizuri na katika msimamo ipo katika nafasi nzuri"

"Lengo letu ni  kufanya vizuri mkakati na mchakato tuliouanzisha kwa kutumia mfumo wetu wa kupapasa" Alisema Bwire.

Hali ya Wachezaji.

Akielezea hali za wachezaji , amesema kuwa wachezaji wote kwa sasa wapo vizuri na hakuna mchzeji mwenye majuruhi ya kumfanya asifike uwanjani.

Join us on WHATSAPP Usipitwe Na Breaking News Za Soka: Jiunge nasi kupitia Facebook, Bofya LIKE Button...

No comments:

Note: only a member of this blog may post a comment.