Chirwa Kutimukia Simba Kila Kitu Wazi Sasa.


Straika wa Yanga, Obrey Chirwa yupo tayari kujiunga na wekundu wa msimbazi 'Simba'' ifikapo mwisho wa msimu huu wa Ligi Kuu Bara.

Mkataba wa mshambuliaji huyo kuendelea kuitumikia Yanga unamalizika msimu huu na tayari ameweka bayana ya kuwa yupo tayari kutua kunako mitaa ya Msimbazi.

Kwa mujibu wa chanzo kikichoripoti taarifa hii kinaeleza kuwa mkataba unamruhusu kuondoka Yanga na hii ni kutokana na kuyumba kwa uchumi na pia kimeweka bayana kiwa uongozi wa Yanga tayari umeanza mazungumzo ya kuhakikisha unambakisha Chirwa Jangwani.

Chanzo hicho kiliendelea, inaamika kuwa kwa sasa tayari Chirwa ameshasaini mkataba wa makubaliano na Simba kitu ambacho kinaelezwa kuwa sababu za yeye kukosa penati.

Source: goal.

No comments:

Note: only a member of this blog may post a comment.