NANI ATAPAPASWA HAPO KESHO?

Na Joseph michael
Kuelekea pambano la watani wa jadi nchini Tanzania, Simba SC na Yanga FC Jumapili Aprili 29, 2018 nani atapapaswa? Hili ndo swali ambalo linagonga vichwa vya habari upande wa mchezo wa soka kwa wanachama, mashabiki, na wadau mbalimbali wa michezo.

Timu zote mbili Simba na Yanga zimeamua kuweka kambi katika mji wa Morogoro kujiandaa na mchezo ujao wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL), Jumapili wiki hii kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.

Simba waliwasili Morogoro wakitokea Iringa ambako wakikipiga na Lipuli FC katika mfululizo wa ligi hiyo ya VPL na kulazimishwa sare ya 1-1 kwenye uwanja wa Samora.

Yanga walitokea mkoani Mbeya ambako walicheza mechi ya ligi hiyo na kutoka sare ya 1-1 na wenyeji Mbeya City.

Mchezo wa Jumapili unatarajiwa kuwa mkali na wa kusisimua ambapo Simba watahitaji kushinda ili kujisafishia njia ya ubingwa wakiwa sasa ndo vinara wa (VPL) kwa alama 59 baada ya kucheza mechi 25. Huku Yanga ikawa ya pili kwenye msimamo kwa alama 48 kwa mchezo 23.

Yanga inazidiwa alama 11 na Simba licha ya Yanga kuwa viporo viwili, maana yake ni kwamba ili kutetea ubingwa itabidi washinde Jumapili na washinde mechi zote zilizobaki za ligi kuu, huku wakiwaombea mahasimu wao wapoteze mechi moja. Tukutane uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam April29 tushuhudie yatakayojiri.

Credit:mwanaspoti

No comments:

Note: only a member of this blog may post a comment.